11. Je! Utulizi wa Mungu ni mdogo sana kwako,Na hilo neno la upole si kitu kwako?
12. Mbona moyo wako unakutaharakisha!Na macho yako, je! Kwani kung’ariza?
13. Hata ukageuza roho yako iwe kinyume cha Mungu,Na kuyatoa maneno kama hayo kinywani mwako.
14. Je! Mwanadamu ni kitu gani, hata akawa safi?Huyo aliyezaliwa na mwanamke, hata awe na haki?
15. Yeye hawategemei watakatifu wake;Naam, mbingu nazo si safi machoni pake.
16. Sembuse mtu ambaye ni mwenye kuchukiza na uchafu,Mwanadamu anywaye uovu kama anywavyo maji!
17. Mimi nitakuonyesha, unisikilize;Na hayo yote niliyoyaona nitayanena;
18. (Ambayo watu wenye hekima wameyatangazaTokea baba zao, wala hawakuyaficha;
19. Waliopewa hiyo nchi peke yao,Wala mgeni hakupita kati yao);
20. Mtu mwovu huwa na uchungu siku zake zote,Hata hesabu ya miaka aliyowekewa mwenye kuonea.
21. Sauti za utisho zi masikioni mwake;Katika kufanikiwa kwake mtekaji nyara atamjia juu yake;
22. Yeye hasadiki kwamba atarudi kutoka gizani,Naye hungojewa na upanga;
23. Hutanga-tanga ili apate chakula, akisema, Ki wapi?Ajua kwamba siku ya giza i tayari karibu yake;
24. Mateso na dhiki humtia hofu;Humshinda kama vile mfalme aliye tayari kwa vita;
25. Kwa kuwa amenyosha mkono wake juu ya Mungu,Na kuendelea kwa kiburi kinyume cha Mwenyezi;
26. Humshambulia na shingo ngumu,Kwa mafundo makubwa ya ngao zake;
27. Kwa kuwa amefunika uso wake na kunona kwake,Na kuwandisha mafuta kiunoni mwake;Naye amekaa katika miji iliyo ukiwa,
28. Katika nyumba ambazo hapana mtu azikaaye,Zilizokuwa tayari kuwa magofu.
29. Hatakuwa tajiri, wala mali zake hazitadumu,Wala maongeo yao hayatainama nchi.