15. Wewe ungeita, nami ningekujibu;Ungekuwa na tamaa ya kazi ya mikono yako.
16. Lakini sasa wazihesabu hatua zangu;Je! Huchungulii dhambi yangu?
17. Kosa langu limetiwa muhuri mfukoni,Nawe waufunga uovu wangu.
18. Lakini, tazama, mlima ukianguka hutoweka,Nalo jabali huondolewa mahali pake;
19. Maji mengi huyapunguza mawe;Mafuriko yake huuchukua mchanga wa nchi;Nawe matumaini ya wanadamu wayaangamiza.
20. Wewe wamshinda nguvu sikuzote, naye hupita aende zakeWabadili sura zake, na kumpeleka aondoke.
21. Wanawe hufikilia heshima, wala yeye hajui;Kisha wao huaibishwa, lakini yeye hana habari zao.
22. Lakini mwili ulio juu yake una maumivu,Na nafsi yake ndani huomboleza.