21. Uondoe mkono wako usinilemee;Na utisho wako usinitie hofu.
22. Basi uite wakati huo, nami nitaitika;Au, niache ninene mimi, nawe unijibu.
23. Maovu yangu na dhambi zangu ni ngapi?Nijulishe kosa langu na dhambi yangu.
24. Mbona umeuficha uso wako,Na kunihesabu kuwa ni adui yako?
25. Je! Utalitaabisha jani lipeperushwalo?Au, je! Utayafuatia hayo mabua makavu?
26. Kwani umeandika maneno ya uchungu juu yangu,Na kunirithisha maovu ya ujana wangu;