19. Yuko nani atakayeshindana nami?Maana sasa nitanyamaa kimya na kutoa roho.
20. Lakini msinifanyie mambo mawili, hayo tu,Ndipo nami sitajificha usoni pako;
21. Uondoe mkono wako usinilemee;Na utisho wako usinitie hofu.
22. Basi uite wakati huo, nami nitaitika;Au, niache ninene mimi, nawe unijibu.
23. Maovu yangu na dhambi zangu ni ngapi?Nijulishe kosa langu na dhambi yangu.