13. Nyamazeni, niacheni, ili nipate kunena,Na hayo yatakayonijilia na yaje.
14. Nitaitwaa nyama ya mwili wangu katika meno yangu,Na kuutwaa uhai wangu mkononi mwangu!
15. Tazama, ataniua; sina tumaini;Ila hata hivyo nitaithibitisha njia yangu mbele yake.
16. Hili nalo litakuwa ni wokovu wangu;Kwani asiyemcha Mungu hatakaribia mbele yake.
17. Sikieni sana maneno yangu,Maelezo yangu na yaingie masikioni mwenu.
18. Angalieni sasa, nimekwisha kulitengeneza neno langu,Najua ya kuwa ni mwenye haki mimi.