10. Hakika atawakemea ninyi,Mkiwapendelea watu kwa siri.
11. Je! Huo ukuu wake hautawatia hofu,Na utisho wake hautawaangukia?
12. Matamko yenu ya hekima ni mithali ya majivu,Ngome zenu ni ngome za udongo.
13. Nyamazeni, niacheni, ili nipate kunena,Na hayo yatakayonijilia na yaje.
14. Nitaitwaa nyama ya mwili wangu katika meno yangu,Na kuutwaa uhai wangu mkononi mwangu!
15. Tazama, ataniua; sina tumaini;Ila hata hivyo nitaithibitisha njia yangu mbele yake.
16. Hili nalo litakuwa ni wokovu wangu;Kwani asiyemcha Mungu hatakaribia mbele yake.
17. Sikieni sana maneno yangu,Maelezo yangu na yaingie masikioni mwenu.
18. Angalieni sasa, nimekwisha kulitengeneza neno langu,Najua ya kuwa ni mwenye haki mimi.
19. Yuko nani atakayeshindana nami?Maana sasa nitanyamaa kimya na kutoa roho.
20. Lakini msinifanyie mambo mawili, hayo tu,Ndipo nami sitajificha usoni pako;