1. Tazama, jicho langu limeyaona hayo yote,Sikio langu limeyasikia na kuelewa nayo.
2. Hayo myajuayo ninyi, na mimi pia nayajua;Mimi si duni kuliko ninyi.
3. Hakika ningenena naye huyo Mwenyezi,Nami nataka kuhojiana na Mungu.
4. Lakini ninyi hubuni maneno ya uongo,Ninyi nyote ni matabibu wasiofaa.
5. Laiti mngenyamaza kabisa!Hilo lingekuwa hekima kwenu.
6. Sikieni sasa basi hoja zangu,Mkayasikie mashindano ya midomo yangu.
7. Je! Mtanena yasiyo ya haki kwa ajili ya Mungu,Na kusema kwa udanganyifu kwa ajili yake?
8. Je! Mtamwonyesha yeye upendeleo?Mtamtetea Mungu?
9. Je! Itafaa yeye kuwatafuta ninyi?Au, kama kumdanganya mtu, je! Mtamdanganya yeye?
10. Hakika atawakemea ninyi,Mkiwapendelea watu kwa siri.