Ayu. 11:5-14 Swahili Union Version (SUV)

5. Lakini, laiti Mungu angenena,Na kuifunua midomo yake juu yako;

6. Tena akuonyeshe hizo siri za hekima,Ya kuwa hufanikiwa katika kuyatimiza makusudi yake!Ujue basi ya kuwa Mungu akuachilia katika uovu wako.

7. Je! Wewe waweza kuuvumbua ukuu wa Mungu?Waweza kuufikilia upeo wa huyo Mwenyezi?

8. Ni juu mno kama mbingu; waweza kufanya nini wewe?Ni wenye kina kuliko kuzimuni; waweza kujua nini wewe?

9. Cheo chake ni kirefu kuliko dunia,Ni kipana zaidi ya bahari.

10. Yeye akipita, na kufunga watu,Na kuwaita hukumuni, ni nani basi awezaye kumzuia?

11. Kwani yeye awajua watu baradhuli;Huona na uovu pia, hata asipoufikiri.

12. Lakini mpumbavu aweza kupata ufahamu,Ingawa mwanadamu huzaliwa kama mtoto wa punda-mwitu.

13. Wewe ukiuweka moyo wako kwa uelekevu,Na kumnyoshea mikono yako;

14. Ikiwa una uovu mkononi mwako, uweke mbali nawe,Wala usikubali upuzi kukaa hemani mwako;

Ayu. 11