Ayu. 11:11-16 Swahili Union Version (SUV)

11. Kwani yeye awajua watu baradhuli;Huona na uovu pia, hata asipoufikiri.

12. Lakini mpumbavu aweza kupata ufahamu,Ingawa mwanadamu huzaliwa kama mtoto wa punda-mwitu.

13. Wewe ukiuweka moyo wako kwa uelekevu,Na kumnyoshea mikono yako;

14. Ikiwa una uovu mkononi mwako, uweke mbali nawe,Wala usikubali upuzi kukaa hemani mwako;

15. Hakika ndipo utakapopata kuinua uso pasipo ila;Naam, utathibitika, wala hutakuwa na hofu;

16. Kwa kuwa utasahau mashaka yako;Utayakumbuka kama maji yaliyokwisha pita;

Ayu. 11