12. Umenijazi uhai na upendeleo,Na maangalizi yako yameilinda roho yangu.
13. Lakini mambo haya uliyaficha moyoni mwako;Najua kuwa haya yamo nafsini mwako;
14. Nikifanya dhambi, ndipo waniangalia,Wala hutaniachilia na uovu wangu.
15. Mimi nikiwa mbaya, ole wangu!Nami nikiwa mwenye haki, walakini sitainua kichwa changu;Mimi nimejaa aibuNa kuyaangalia mateso yangu.
16. Kichwa changu kikijiinua, waniwinda kama simba;Tena wajionyesha kwangu kuwa wa ajabu.
17. Wewe warejeza upya hao mashahidi yako juu yangu,Na kasirani yako waiongeza juu yangu;Jeshi kwa jeshi juu yangu.
18. Kwa nini basi kunitoa tumboni?Ningekata roho, lisinione jicho lo lote.