Amu. 5:5-8 Swahili Union Version (SUV)

5. Milima ikayeyuka mbele za uso wa BWANA,Naam hata Sinai ule mbele za uso wa BWANA, Mungu wa Israeli.

6. Katika siku za Shamgari, mwana wa Anathi,Siku za Yaeli, njia kuu zilikuwa hazina watu;Nao wenye kusafiri walipita kwa njia za kando.

7. Maliwali walikoma katika Israeli, walikoma,Hata mimi Debora nilipoinuka,Nilipoinuka mimi, mama katika Israeli.

8. Walichagua miungu mipya,Ndipo kulikuwa na vita malangoni;Je! Ilionekana ngao au mkukiKatika watu elfu arobaini wa Israeli?

Amu. 5