2 Sam. 23:1-3 Swahili Union Version (SUV)

1. Basi haya ndiyo maneno ya mwisho ya Daudi.Daudi, mwana wa Yese, anena,Anena huyo mtu aliyeinuliwa juu,Yeye, masihi wake Mungu wa Yakobo,Mtungaji wa nyimbo za Israeli mwenye kupendeza;

2. Roho ya BWANA ilinena ndani yangu,Na neno lake likawa ulimini mwangu.

3. Mungu wa Israeli alisema,Mwamba wa Israeli aliniambia,Atawalaye wanadamu kwa haki,Akitawala katika kicho cha Mungu,

2 Sam. 23