47. BWANA ndiye aliye hai;Na ahimidiwe mwamba wangu;Na atukuzwe Mungu wa mwamba wa wokovu wangu;
48. Naam, Mungu anipatiaye kisasi,Na kuwatweza watu chini yangu,
49. Na kunileta nje nitoke kwa adui zangu;Naam, waniinua juu yao walioniinukia;Waniponya na mtu wa jeuri.
50. Basi, BWANA, nitakushukuru kati ya mataifa,Nami nitaliimbia jina lako.
51. Ampa mfalme wake wokovu mkuu;Amfanyia fadhili masihi wake,Daudi na mzao wake, hata milele.