40. Maana umenifunga mshipi wa nguvu kwa vita;Umenitiishia chini yangu walioniondokea.
41. Naam, adui zangu umewafanya wanipe visogo,Ili niwakatilie mbali wanaonichukia.
42. Walitazama, lakini hakuna wa kuokoa;Walimwita BWANA, lakini hakuwajibu.
43. Ndipo nikawaponda kama mavumbi ya nchi,Nikawakanyaga kama matope ya njiani, nikawatawanya.
44. Nawe umeniokoa na mashindano ya watu wangu;Umenihifadhi niwe kichwa cha mataifa;Watu nisiowajua watanitumikia.
45. Wageni watanijia wakinyenyekea;Kwa kusikia tu habari zangu,Mara watanitii.