2 Sam. 22:36-46 Swahili Union Version (SUV)

36. Nawe umenipa ngao ya wokovu wako;Na unyenyekevu wako umenikuza.

37. Umezifanyizia nafasi hatua zangu,Wala miguu yangu haikuteleza.

38. Nimewafuatia adui zangu, na kuwaangamiza;Wala sikurudi nyuma hata walipokomeshwa.

39. Nami nimewakomesha na kuwapiga-piga wasiweze kusimama;Naam, wameanguka chini ya miguu yangu.

40. Maana umenifunga mshipi wa nguvu kwa vita;Umenitiishia chini yangu walioniondokea.

41. Naam, adui zangu umewafanya wanipe visogo,Ili niwakatilie mbali wanaonichukia.

42. Walitazama, lakini hakuna wa kuokoa;Walimwita BWANA, lakini hakuwajibu.

43. Ndipo nikawaponda kama mavumbi ya nchi,Nikawakanyaga kama matope ya njiani, nikawatawanya.

44. Nawe umeniokoa na mashindano ya watu wangu;Umenihifadhi niwe kichwa cha mataifa;Watu nisiowajua watanitumikia.

45. Wageni watanijia wakinyenyekea;Kwa kusikia tu habari zangu,Mara watanitii.

46. Wageni nao watatepetea,Watatoka katika ngome zao wakitetemeka.

2 Sam. 22