2 Sam. 22:34-40 Swahili Union Version (SUV)

34. Huifanya miguu yangu kuwa kama ya kulungu;Na kunisimamisha mahali pangu pa juu.

35. Ananifundisha mikono yangu vita;Hata mikono yangu yaupinda upinde wa shaba.

36. Nawe umenipa ngao ya wokovu wako;Na unyenyekevu wako umenikuza.

37. Umezifanyizia nafasi hatua zangu,Wala miguu yangu haikuteleza.

38. Nimewafuatia adui zangu, na kuwaangamiza;Wala sikurudi nyuma hata walipokomeshwa.

39. Nami nimewakomesha na kuwapiga-piga wasiweze kusimama;Naam, wameanguka chini ya miguu yangu.

40. Maana umenifunga mshipi wa nguvu kwa vita;Umenitiishia chini yangu walioniondokea.

2 Sam. 22