33. Mungu ndiye ngome yangu yenye nguvu;Naye huwaongoza wakamilifu katika njia yake.
34. Huifanya miguu yangu kuwa kama ya kulungu;Na kunisimamisha mahali pangu pa juu.
35. Ananifundisha mikono yangu vita;Hata mikono yangu yaupinda upinde wa shaba.
36. Nawe umenipa ngao ya wokovu wako;Na unyenyekevu wako umenikuza.
37. Umezifanyizia nafasi hatua zangu,Wala miguu yangu haikuteleza.