2 Sam. 22:31-35 Swahili Union Version (SUV)

31. Mungu njia yake ni kamilifu;Ahadi ya BWANA imehakikishwa;Yeye ndiye ngao yaoWote wanaomkimbilia.

32. Maana ni nani aliye Mungu, ila BWANA?Ni nani aliye mwamba, ila Mungu wetu?

33. Mungu ndiye ngome yangu yenye nguvu;Naye huwaongoza wakamilifu katika njia yake.

34. Huifanya miguu yangu kuwa kama ya kulungu;Na kunisimamisha mahali pangu pa juu.

35. Ananifundisha mikono yangu vita;Hata mikono yangu yaupinda upinde wa shaba.

2 Sam. 22