2 Sam. 22:27-43 Swahili Union Version (SUV)

27. Kwake ajitakasaye utajionyesha kuwa mtakatifu;Na kwa mpotovu utajionyesha kuwa mkaidi.

28. Na watu wanaoonewa wewe utawaokoa;Ila macho yako ni juu ya wenye kiburi, uwadhili.

29. Kwa kuwa wewe u taa yangu, Ee BWANA;Na BWANA ataniangazia giza langu.

30. Maana kwa msaada wako nafuatia jeshi;Kwa msaada wa Mungu wangu naruka ukuta.

31. Mungu njia yake ni kamilifu;Ahadi ya BWANA imehakikishwa;Yeye ndiye ngao yaoWote wanaomkimbilia.

32. Maana ni nani aliye Mungu, ila BWANA?Ni nani aliye mwamba, ila Mungu wetu?

33. Mungu ndiye ngome yangu yenye nguvu;Naye huwaongoza wakamilifu katika njia yake.

34. Huifanya miguu yangu kuwa kama ya kulungu;Na kunisimamisha mahali pangu pa juu.

35. Ananifundisha mikono yangu vita;Hata mikono yangu yaupinda upinde wa shaba.

36. Nawe umenipa ngao ya wokovu wako;Na unyenyekevu wako umenikuza.

37. Umezifanyizia nafasi hatua zangu,Wala miguu yangu haikuteleza.

38. Nimewafuatia adui zangu, na kuwaangamiza;Wala sikurudi nyuma hata walipokomeshwa.

39. Nami nimewakomesha na kuwapiga-piga wasiweze kusimama;Naam, wameanguka chini ya miguu yangu.

40. Maana umenifunga mshipi wa nguvu kwa vita;Umenitiishia chini yangu walioniondokea.

41. Naam, adui zangu umewafanya wanipe visogo,Ili niwakatilie mbali wanaonichukia.

42. Walitazama, lakini hakuna wa kuokoa;Walimwita BWANA, lakini hakuwajibu.

43. Ndipo nikawaponda kama mavumbi ya nchi,Nikawakanyaga kama matope ya njiani, nikawatawanya.

2 Sam. 22