27. Kwake ajitakasaye utajionyesha kuwa mtakatifu;Na kwa mpotovu utajionyesha kuwa mkaidi.
28. Na watu wanaoonewa wewe utawaokoa;Ila macho yako ni juu ya wenye kiburi, uwadhili.
29. Kwa kuwa wewe u taa yangu, Ee BWANA;Na BWANA ataniangazia giza langu.
30. Maana kwa msaada wako nafuatia jeshi;Kwa msaada wa Mungu wangu naruka ukuta.
31. Mungu njia yake ni kamilifu;Ahadi ya BWANA imehakikishwa;Yeye ndiye ngao yaoWote wanaomkimbilia.
32. Maana ni nani aliye Mungu, ila BWANA?Ni nani aliye mwamba, ila Mungu wetu?
33. Mungu ndiye ngome yangu yenye nguvu;Naye huwaongoza wakamilifu katika njia yake.
34. Huifanya miguu yangu kuwa kama ya kulungu;Na kunisimamisha mahali pangu pa juu.
35. Ananifundisha mikono yangu vita;Hata mikono yangu yaupinda upinde wa shaba.
36. Nawe umenipa ngao ya wokovu wako;Na unyenyekevu wako umenikuza.
37. Umezifanyizia nafasi hatua zangu,Wala miguu yangu haikuteleza.
38. Nimewafuatia adui zangu, na kuwaangamiza;Wala sikurudi nyuma hata walipokomeshwa.
39. Nami nimewakomesha na kuwapiga-piga wasiweze kusimama;Naam, wameanguka chini ya miguu yangu.
40. Maana umenifunga mshipi wa nguvu kwa vita;Umenitiishia chini yangu walioniondokea.
41. Naam, adui zangu umewafanya wanipe visogo,Ili niwakatilie mbali wanaonichukia.
42. Walitazama, lakini hakuna wa kuokoa;Walimwita BWANA, lakini hakuwajibu.
43. Ndipo nikawaponda kama mavumbi ya nchi,Nikawakanyaga kama matope ya njiani, nikawatawanya.