2 Sam. 22:21-34 Swahili Union Version (SUV)

21. BWANA alinitendea sawasawa na haki yangu;Sawasawa na usafi wa mikono yangu akanilipa.

22. Maana nimezishika njia za BWANA,Wala sikumwasi Mungu wangu.

23. Maana hukumu zake zote zilikuwa mbele yangu;Na kwa habari za amri zake, sikuziacha.

24. Nami nalikuwa mkamilifu kwake,Nikajilinda na uovu wangu.

25. Basi BWANA amenilipa sawasawa na haki yangu;Sawasawa na usafi wa mikono yangu mbele zake.

26. Kwa mtu mwenye fadhili utakuwa mwenye fadhiliKwa mkamilifu utajionyesha kuwa mkamilifu;

27. Kwake ajitakasaye utajionyesha kuwa mtakatifu;Na kwa mpotovu utajionyesha kuwa mkaidi.

28. Na watu wanaoonewa wewe utawaokoa;Ila macho yako ni juu ya wenye kiburi, uwadhili.

29. Kwa kuwa wewe u taa yangu, Ee BWANA;Na BWANA ataniangazia giza langu.

30. Maana kwa msaada wako nafuatia jeshi;Kwa msaada wa Mungu wangu naruka ukuta.

31. Mungu njia yake ni kamilifu;Ahadi ya BWANA imehakikishwa;Yeye ndiye ngao yaoWote wanaomkimbilia.

32. Maana ni nani aliye Mungu, ila BWANA?Ni nani aliye mwamba, ila Mungu wetu?

33. Mungu ndiye ngome yangu yenye nguvu;Naye huwaongoza wakamilifu katika njia yake.

34. Huifanya miguu yangu kuwa kama ya kulungu;Na kunisimamisha mahali pangu pa juu.

2 Sam. 22