2 Sam. 22:18-22 Swahili Union Version (SUV)

18. Akaniokoa na adui yangu mwenye nguvu,Na wale walionichukia;Maana walikuwa na nguvu kuliko mimi.

19. Walinikabili siku ya msiba wangu;Lakini BWANA alikuwa tegemeo langu.

20. Akanitoa akanipeleka panapo nafasi;Aliniponya kwa kuwa alipendezwa nami.

21. BWANA alinitendea sawasawa na haki yangu;Sawasawa na usafi wa mikono yangu akanilipa.

22. Maana nimezishika njia za BWANA,Wala sikumwasi Mungu wangu.

2 Sam. 22