18. Akaniokoa na adui yangu mwenye nguvu,Na wale walionichukia;Maana walikuwa na nguvu kuliko mimi.
19. Walinikabili siku ya msiba wangu;Lakini BWANA alikuwa tegemeo langu.
20. Akanitoa akanipeleka panapo nafasi;Aliniponya kwa kuwa alipendezwa nami.
21. BWANA alinitendea sawasawa na haki yangu;Sawasawa na usafi wa mikono yangu akanilipa.
22. Maana nimezishika njia za BWANA,Wala sikumwasi Mungu wangu.