2 Sam. 22:13-27 Swahili Union Version (SUV)

13. Toka mwangaza uliokuwa mbele zakeMakaa ya moto yakawashwa.

14. BWANA alipiga radi toka mbinguni,Naye Aliye juu akaitoa sauti yake.

15. Akapiga mishale, akawatawanya;Umeme, naye akawatapanya.

16. Ndipo ilipoonekana mikondo ya bahari,Misingi ya ulimwengu ikafichuliwa,Kwa kukemea kwake BWANA,Kwa mvumo wa pumzi ya puani mwake.

17. Alipeleka kutoka juu, akanishika;Akanitoa katika maji mengi;

18. Akaniokoa na adui yangu mwenye nguvu,Na wale walionichukia;Maana walikuwa na nguvu kuliko mimi.

19. Walinikabili siku ya msiba wangu;Lakini BWANA alikuwa tegemeo langu.

20. Akanitoa akanipeleka panapo nafasi;Aliniponya kwa kuwa alipendezwa nami.

21. BWANA alinitendea sawasawa na haki yangu;Sawasawa na usafi wa mikono yangu akanilipa.

22. Maana nimezishika njia za BWANA,Wala sikumwasi Mungu wangu.

23. Maana hukumu zake zote zilikuwa mbele yangu;Na kwa habari za amri zake, sikuziacha.

24. Nami nalikuwa mkamilifu kwake,Nikajilinda na uovu wangu.

25. Basi BWANA amenilipa sawasawa na haki yangu;Sawasawa na usafi wa mikono yangu mbele zake.

26. Kwa mtu mwenye fadhili utakuwa mwenye fadhiliKwa mkamilifu utajionyesha kuwa mkamilifu;

27. Kwake ajitakasaye utajionyesha kuwa mtakatifu;Na kwa mpotovu utajionyesha kuwa mkaidi.

2 Sam. 22