2 Sam. 22:12-19 Swahili Union Version (SUV)

12. Akafanya giza hema zake za kumzunguka,Makusanyiko ya maji, mawingu makuu ya mbinguni.

13. Toka mwangaza uliokuwa mbele zakeMakaa ya moto yakawashwa.

14. BWANA alipiga radi toka mbinguni,Naye Aliye juu akaitoa sauti yake.

15. Akapiga mishale, akawatawanya;Umeme, naye akawatapanya.

16. Ndipo ilipoonekana mikondo ya bahari,Misingi ya ulimwengu ikafichuliwa,Kwa kukemea kwake BWANA,Kwa mvumo wa pumzi ya puani mwake.

17. Alipeleka kutoka juu, akanishika;Akanitoa katika maji mengi;

18. Akaniokoa na adui yangu mwenye nguvu,Na wale walionichukia;Maana walikuwa na nguvu kuliko mimi.

19. Walinikabili siku ya msiba wangu;Lakini BWANA alikuwa tegemeo langu.

2 Sam. 22