2 Sam. 22:11-25 Swahili Union Version (SUV)

11. Akapanda juu ya kerubi akaruka;Naam, alionekana juu ya mabawa ya upepo.

12. Akafanya giza hema zake za kumzunguka,Makusanyiko ya maji, mawingu makuu ya mbinguni.

13. Toka mwangaza uliokuwa mbele zakeMakaa ya moto yakawashwa.

14. BWANA alipiga radi toka mbinguni,Naye Aliye juu akaitoa sauti yake.

15. Akapiga mishale, akawatawanya;Umeme, naye akawatapanya.

16. Ndipo ilipoonekana mikondo ya bahari,Misingi ya ulimwengu ikafichuliwa,Kwa kukemea kwake BWANA,Kwa mvumo wa pumzi ya puani mwake.

17. Alipeleka kutoka juu, akanishika;Akanitoa katika maji mengi;

18. Akaniokoa na adui yangu mwenye nguvu,Na wale walionichukia;Maana walikuwa na nguvu kuliko mimi.

19. Walinikabili siku ya msiba wangu;Lakini BWANA alikuwa tegemeo langu.

20. Akanitoa akanipeleka panapo nafasi;Aliniponya kwa kuwa alipendezwa nami.

21. BWANA alinitendea sawasawa na haki yangu;Sawasawa na usafi wa mikono yangu akanilipa.

22. Maana nimezishika njia za BWANA,Wala sikumwasi Mungu wangu.

23. Maana hukumu zake zote zilikuwa mbele yangu;Na kwa habari za amri zake, sikuziacha.

24. Nami nalikuwa mkamilifu kwake,Nikajilinda na uovu wangu.

25. Basi BWANA amenilipa sawasawa na haki yangu;Sawasawa na usafi wa mikono yangu mbele zake.

2 Sam. 22