2 Sam. 20:23-26 Swahili Union Version (SUV)

23. Basi Yoabu alikuwa juu ya jeshi lote la Israeli; na Benaya, mwana wa Yehoyada, alikuwa juu ya Wakerethi, na juu ya Wapelethi;

24. na Adoramu alikuwa juu ya shokoa; na Yehoshafati, mwana wa Ahiludi, alikuwa mkumbushi;

25. na Shausha mwandishi; na Sadoki na Abiathari walikuwa makuhani.

26. Tena na Ira, Myairi, alikuwa kuhani kwa Daudi.

2 Sam. 20