23. Basi Yoabu alikuwa juu ya jeshi lote la Israeli; na Benaya, mwana wa Yehoyada, alikuwa juu ya Wakerethi, na juu ya Wapelethi;
24. na Adoramu alikuwa juu ya shokoa; na Yehoshafati, mwana wa Ahiludi, alikuwa mkumbushi;
25. na Shausha mwandishi; na Sadoki na Abiathari walikuwa makuhani.
26. Tena na Ira, Myairi, alikuwa kuhani kwa Daudi.