1. Ikawa miaka ishirini ilipopita, ambayo katika hiyo Sulemani aliijenga nyumba ya BWANA, na nyumba yake mwenyewe;
2. ndipo Sulemani akaijenga miji ile Hiramu aliyompa Sulemani, akawakalisha humo wana wa Israeli.
3. Naye Sulemani akaenda Hamath-zoba, akaushinda.
4. Akaujenga Tadmori wa nyikani, na miji yote ya hazina, aliyoijenga katika Hamathi.