2 Nya. 8:1-4 Swahili Union Version (SUV)

1. Ikawa miaka ishirini ilipopita, ambayo katika hiyo Sulemani aliijenga nyumba ya BWANA, na nyumba yake mwenyewe;

2. ndipo Sulemani akaijenga miji ile Hiramu aliyompa Sulemani, akawakalisha humo wana wa Israeli.

3. Naye Sulemani akaenda Hamath-zoba, akaushinda.

4. Akaujenga Tadmori wa nyikani, na miji yote ya hazina, aliyoijenga katika Hamathi.

2 Nya. 8