2 Nya. 13:17-20 Swahili Union Version (SUV)

17. Abiya na watu wake wakawapiga mapigo makuu; hata wakaanguka wameuawa wa Israeli mia tano elfu, watu wateule.

18. Ndivyo walivyotiishwa wana wa Israeli wakati ule, wakashinda wana wa Yuda, kwa kuwa walimtegemea BWANA, Mungu wa baba zao.

19. Abiya akamfuata Yeroboamu, akamnyang’anya miji, Betheli na miji yake, na Yeshana na miji yake, na Efroni na miji yake.

20. Wala Yeroboamu hakupata nguvu tena siku za Abiya; kisha BWANA akampiga, akafa.

2 Nya. 13