2 Nya. 11:5-13 Swahili Union Version (SUV)

5. Naye Rehoboamu akakaa Yerusalemu, akajenga miji yenye ngome katika Yuda.

6. Akajenga na Bethlehemu, na Etamu, na Tekoa,

7. na Bethsuri, na Soko, na Adulamu,

8. na Gathi, na Maresha, na Zifu,

9. na Adoraimu, na Lakishi, na Azeka,

10. na Sora, na Aiyaloni, na Hebroni, iliyoko katika Yuda na Benyamini, miji yenye maboma.

11. Akazifanya imara hizo ngome, akaweka majemadari humo, na akiba ya vyakula, na mafuta, na mvinyo.

12. Na ndani ya miji yote mmoja mmoja aliweka ngao na mikuki, akaifanya kuwa na nguvu nyingi mno. Yuda na Benyamini ikawa milki yake.

13. Wakamwendea makuhani na Walawi waliokuwa katika Israeli yote, kutoka mpaka wao wote.

2 Nya. 11