2 Nya. 10:17-19 Swahili Union Version (SUV)

17. Lakini kwa habari za wana wa Israeli waliokaa katika miji ya Yuda, Rehoboamu alitawala juu yao.

18. Ndipo mfalme Rehoboamu akamtuma Adoramu, msimamizi wa shokoa; nao wana wa Israeli wakamtupia mawe, hata akafa. Mfalme Rehoboamu akafanya haraka kupanda garini mwake, ili akimbilie Yerusalemu.

19. Hivyo Israeli wakaasi juu ya nyumba ya Daudi, hata leo.

2 Nya. 10