2 Kor. 3:11-15 Swahili Union Version (SUV)

11. Kwa maana, ikiwa ile inayobatilika ilikuwa na utukufu, zaidi sana ile ikaayo ina utukufu.

12. Basi, kwa kuwa mna taraja la namna hii, twatumia ujasiri mwingi;

13. nasi si kama Musa alivyotia utaji juu ya uso wake, ili kwamba Waisraeli wasitazame sana mwisho wa ile iliyokuwa ikibatilika;

14. ila fikira zao zilitiwa uzito. Kwa maana hata leo hivi, wakati lisomwapo Agano la Kale, utaji uo huo wakaa; yaani, haikufunuliwa kwamba huondolewa katika Kristo;

15. ila hata leo, torati ya Musa isomwapo, utaji huikalia mioyo yao.

2 Kor. 3