2 Fal. 15:1-4 Swahili Union Version (SUV)

1. Katika mwaka wa ishirini na saba wa Yeroboamu mfalme wa Israeli Uzia mwana wa Amazia mfalme wa Yuda akaanza kutawala.

2. Alikuwa na umri wa miaka kumi na sita alipoanza kutawala; akatawala miaka hamsini na miwili huko Yerusalemu. Na jina la mamaye aliitwa Yekolia wa Yerusalemu.

3. Akafanya yaliyo mema machoni pa BWANA, kama yote aliyoyafanya babaye Amazia.

4. Ila mahali pa juu hapakuondolewa, nao watu wakaendelea kutoa sadaka na kufukiza uvumba katika mahali pa juu.

2 Fal. 15