1 Yoh. 3:1-3 Swahili Union Version (SUV)

1. Tazameni, ni pendo la namna gani alilotupa Baba, kwamba tuitwe wana wa Mungu; na ndivyo tulivyo. Kwa sababu hii ulimwengu haututambui, kwa kuwa haukumtambua yeye.

2. Wapenzi, sasa tu wana wa Mungu, wala haijadhihirika bado tutakavyokuwa; lakini twajua ya kuwa atakapodhihirishwa, tutafanana naye; kwa maana tutamwona kama alivyo.

3. Na kila mwenye matumaini haya katika yeye hujitakasa, kama yeye alivyo mtakatifu.

1 Yoh. 3