23. Kila amkanaye Mwana, hanaye Baba; amkiriye Mwana anaye Baba pia.
24. Ninyi basi, hilo mlilolisikia tangu mwanzo na likae ndani yenu. Ikiwa hilo mlilolisikia tangu mwanzo linakaa ndani yenu, ninyi nanyi mtakaa ndani ya Mwana, na ndani ya Baba.
25. Na hii ndiyo ahadi aliyotuahidia, yaani, uzima wa milele.
26. Nimewaandikia haya katika habari za watu wale wanaotaka kuwapoteza.