1 Tim. 6:18-21 Swahili Union Version (SUV)

18. Watende mema, wawe matajiri kwa kutenda mema, wawe tayari kutoa mali zao, washirikiane na wengine kwa moyo;

19. huku wakijiwekea akiba iwe msingi mzuri kwa wakati ujao, ili wapate uzima ulio kweli kweli.

20. Ee Timotheo, ilinde hiyo amana; ujiepushe na maneno yasiyo ya dini, yasiyo na maana, na mashindano ya elimu iitwayo elimu kwa uongo;

21. ambayo wengine wakiikiri hiyo wameikosa Imani. Neema na iwe pamoja nanyi.

1 Tim. 6