1 Tim. 2:1-4 Swahili Union Version (SUV)

1. Basi, kabla ya mambo yote, nataka dua, na sala, na maombezi, na shukrani, zifanyike kwa ajili ya watu wote;

2. kwa ajili ya wafalme na wote wenye mamlaka, tuishi maisha ya utulivu na amani, katika utauwa wote na ustahivu.

3. Hili ni zuri, nalo lakubalika mbele za Mungu Mwokozi wetu;

4. ambaye hutaka watu wote waokolewe, na kupata kujua yaliyo kweli.

1 Tim. 2