5. Walioshiba wamejikodisha ili kupata chakula,Na hao waliokuwa na njaa wamepata raha.Naam, huyo aliyekua tasa amezaa watoto saba,Na yeye aliye na wana wengi amedhoofika.
6. BWANA huua, naye hufanya kuwa hai;Hushusha hata kuzimu, tena huleta juu.
7. BWANA hufukarisha mtu, naye hutajirisha;Hushusha chini, tena huinua juu.
8. Humwinua mnyonge kutoka mavumbini,Humpandisha mhitaji kutoka jaani,Ili awaketishe pamoja na wakuu,Wakakirithi kiti cha enzi cha utukufu;Kwa maana nguzo za dunia zina BWANA,Naye ameuweka ulimwengu juu yake.
9. Yeye atailinda miguu ya watakatifu wake;Bali waovu watanyamazishwa gizani,Maana kwa nguvu hakuna atakayeshinda;