1 Sam. 2:1-4 Swahili Union Version (SUV)

1. Naye Hana akaomba, akasema,Moyo wangu wamshangilia BWANA,Pembe yangu imetukuka katika BWANA,Kinywa changu kimepanuka juu ya adui zangu;Kwa kuwa naufurahia wokovu wako;

2. Hakuna aliye mtakatifu kama BWANA;Kwa maana hakuna ye yote ila wewe,Wala hakuna mwamba kama Mungu wetu.

3. Msizidi kunena kwa kutakabari hivyo;Majivuno yasitoke vinywani mwenu;Kwa kuwa BWANA ni Mungu wa maarifa,Na matendo hupimwa na yeye kwa mizani.

4. Pinde zao mashujaa zimevunjika,Na hao waliojikwaa wamefungiwa nguvu.

1 Sam. 2