1 Sam. 1:25-28 Swahili Union Version (SUV)

25. Nao wakamchinja huyo ng’ombe, wakamleta mtoto kwa Eli.

26. Akasema, Ee bwana wangu, kama iishivyo roho yako, bwana wangu, mimi ndimi yule mwanamke aliyesimama karibu nawe hapa, nikimwomba BWANA.

27. Naliomba nipewe mtoto huyu; BWANA akanipa dua yangu niliyomwomba;

28. kwa sababu hiyo mimi nami nimempa BWANA mtoto huyu; wakati wote atakaokuwa hai amepewa BWANA. Naye akamwabudu BWANA huko.

1 Sam. 1