1 Sam. 1:14-16 Swahili Union Version (SUV)

14. Ndipo Eli akamwambia, Je! Utakuwa mlevi hata lini? Achilia mbali divai yako.

15. Hana akajibu, akasema, Hasha! Bwana wangu, mimi ni mwanamke mwenye roho ya huzuni, mimi sikunywa divai wala kileo, ila nimeimimina roho yangu mbele za BWANA.

16. Usimdhanie mjakazi wako kuwa ni mwanamke asiyefaa kitu; kwa kuwa katika wingi wa kuugua kwangu na kusikitika kwangu ndivyo nilivyonena hata sasa.

1 Sam. 1