8. Neno la mwisho ni hili; mwe na nia moja, wenye kuhurumiana, wenye kupendana kama ndugu, wasikitikivu, wanyenyekevu;
9. watu wasiolipa baya kwa baya, au laumu kwa laumu; bali wenye kubariki; kwa sababu hayo ndiyo mliyoitiwa ili mrithi baraka.
10. Kwa maana,Atakaye kupenda maisha,Na kuona siku njema,Auzuie ulimi wake usinene mabaya,Na midomo yake isiseme hila.