1 Nya. 7:25-39 Swahili Union Version (SUV)

25. Mwanawe ni Refa, na Reshefu, na mwanawe huyo ni Tela, na mwanawe huyo ni Tahani;

26. na mwanawe huyo ni Ladani, na mwanawe huyo ni Amihudi, na mwanawe huyo ni Elishama;

27. na mwanawe huyo ni Nuni, na mwanawe huyo ni Yoshua.

28. Na hizi ndizo hozi zao na makao yao; Betheli na vijiji vyake, na upande wa mashariki Naara, na upande wa magharibi Gezeri na vijiji vyake; na Shekemu pia na vijiji vyake, hata Aza na vijiji vyake;

29. na mipakani mwa wana wa Manase; Beth-sheani na vijiji vyake; na Taanaki na vijiji vyake; na Megido na vijiji vyake; na Dori na vijiji vyake. Katika miji hiyo walikaa wana wa Yusufu, mwana wa Israeli.

30. Wana wa Asheri; Imna, na Ishva, na Ishvi, na Beria, na umbu lao, Sera.

31. Na wana wa Beria; Heberi, na Malkieli, aliyekuwa babaye Birzaithi.

32. Na Heberi akamzaa Yafleti, na Shomeri, na Hothamu, na umbu lao, Shua.

33. Na wana wa Yafleti; Pasaki, na Bimhali, na Ashvathi. Hao ndio wana wa Yafleti.

34. Na wana wa Shomeri; Ahi, na Roga, na Yehuba, na Aramu.

35. Na wana wa nduguye Helemu; Sofa, na Imna, na Sheleshi, na Amali.

36. Wana wa Sofa; Sua, na Harneferi, na Shuali, na Beri, na Imra;

37. na Bezeri, na Hodu, na Shama, na Shilsha, na Ithrani, na Beera.

38. Na wana wa Yetheri; Yefune, na Pispa, na Ara.

39. Na wana wa Ula; Ara, na Hanieli na Risia.

1 Nya. 7