23. Naye akamwingilia mkewe, naye akachukua mimba na kuzaa mwana, akamwita jina lake Beria, kwa sababu mna mabaya nyumbani mwake.
24. Na binti yake alikuwa Sheera, ambaye alijenga Beth-horoni, wa chini na wa juu, na Uzen-sheera.
25. Mwanawe ni Refa, na Reshefu, na mwanawe huyo ni Tela, na mwanawe huyo ni Tahani;
26. na mwanawe huyo ni Ladani, na mwanawe huyo ni Amihudi, na mwanawe huyo ni Elishama;
27. na mwanawe huyo ni Nuni, na mwanawe huyo ni Yoshua.
28. Na hizi ndizo hozi zao na makao yao; Betheli na vijiji vyake, na upande wa mashariki Naara, na upande wa magharibi Gezeri na vijiji vyake; na Shekemu pia na vijiji vyake, hata Aza na vijiji vyake;
29. na mipakani mwa wana wa Manase; Beth-sheani na vijiji vyake; na Taanaki na vijiji vyake; na Megido na vijiji vyake; na Dori na vijiji vyake. Katika miji hiyo walikaa wana wa Yusufu, mwana wa Israeli.
30. Wana wa Asheri; Imna, na Ishva, na Ishvi, na Beria, na umbu lao, Sera.
31. Na wana wa Beria; Heberi, na Malkieli, aliyekuwa babaye Birzaithi.
32. Na Heberi akamzaa Yafleti, na Shomeri, na Hothamu, na umbu lao, Shua.
33. Na wana wa Yafleti; Pasaki, na Bimhali, na Ashvathi. Hao ndio wana wa Yafleti.
34. Na wana wa Shomeri; Ahi, na Roga, na Yehuba, na Aramu.
35. Na wana wa nduguye Helemu; Sofa, na Imna, na Sheleshi, na Amali.
36. Wana wa Sofa; Sua, na Harneferi, na Shuali, na Beri, na Imra;
37. na Bezeri, na Hodu, na Shama, na Shilsha, na Ithrani, na Beera.