1 Nya. 6:4-17 Swahili Union Version (SUV)

4. Eleazari akamzaa Finehasi; na Finehasi akamzaa Abishua;

5. na Abishua akamzaa Buki; na Buki akamzaa Uzi;

6. na Uzi akamzaa Zerahia; na Zerahia akamzaa Merayothi,

7. na Merayothi akamzaa Amaria; na Amaria akamzaa Ahitubu;

8. na Ahitubu akamzaa Sadoki; na Sadoki akamzaa Ahimaasi;

9. na Ahimaasi akamzaa Azaria; na Azaria akamzaa Yohana;

10. na Yohana akamzaa Azaria (ndiye huyo aliyefanya kazi ya ukuhani katika nyumba aliyoijenga Sulemani huko Yerusalemu)

11. na Azaria akamzaa Amaria; na Amaria akamzaa Ahitubu;

12. na Ahitubu akamzaa Sadoki; na Sadoki akamzaa Meshulamu;

13. na Meshulamu akamzaa Hilkia; na Hilkia akamzaa Azaria;

14. na Azaria akamzaa Seraya; na Seraya akamzaa Yehosadaki;

15. na Yehosadaki akachukuliwa mateka, hapo BWANA alipowachukua mateka Yuda na Yerusalemu, kwa mkono wa Nebukadreza.

16. Wana wa Lawi; Gershoni, na Kohathi, na Merari.

17. Na haya ndiyo majina ya wana wa Gershoni; Libni, na Shimei.

1 Nya. 6