1 Nya. 3:1-7 Swahili Union Version (SUV)

1. Basi hawa ndio wana wa Daudi, aliozaliwa huko Hebroni; Amnoni, mzaliwa wa kwanza, mwana wa Ahinoamu, Myezreeli; wa pili, Danieli, wa Abigaili, Mkarmeli;

2. wa tatu, Absalomu, mwana wa Maaka, binti Talmai, mfalme wa Geshuri; wa nne, Adoniya, mwana wa Hagithi;

3. wa tano, Shefatia, wa Abitali; wa sita, Ithreamu, kwa Egla, mkewe.

4. Sita alizaliwa huko Hebroni; na huko akamiliki miaka saba na miezi sita; na huko Yerusalemu akamiliki miaka thelathini na mitatu.

5. Na hawa alizaliwa huko Yerusalemu; Shamua, na Shobabu, na Nathani, na Sulemani, wanne, wana wa Bathsheba, binti Eliamu;

6. na Ibhari, na Elishua, na Elipeleti;

7. na Noga, na Nefegi, na Yafia;

1 Nya. 3