19. Hizo ndizo zamu za mabawabu; wa wana wa Wakora, na wa wana wa Merari.
20. Na katika Walawi; Ahia alikuwa juu ya hazina za nyumba ya Mungu, na juu ya hazina za vitu vilivyowekwa wakfu.
21. Wana wa Ladani; wana wa Wagershoni waliokuwa wa Ladani; wakuu wa mbari za mababa waliokuwa wa Ladani, Mgershoni; Yehieli.
22. Wana wa Yehieli; Zethamu, na Yoeli nduguye, juu ya hazina za nyumba ya BWANA.
23. Wa Waamramu, wa Waishari, wa Wahebroni, wa Wauzieli;