1 Nya. 23:6-12 Swahili Union Version (SUV)

6. Basi Daudi akawagawanya kuwa zamu zao sawasawa na wana wa Lawi; Gershoni, Kohathi, na Merari.

7. Wa Wagershoni; Ladani, na Shimei.

8. Wana wa Ladani; Yehieli mkuu wao, na Zethamu, na Yoeli, watu watatu.

9. Wana wa Shimei; Shelomothi, na Hazieli, na Harani, watatu. Hao walikuwa vichwa vya mbari za baba za Ladani.

10. Na wana wa Shimei; Yahathi, na Zina, na Yeushi, na Beria. Hao wanne walikuwa wana wa Shimei.

11. Naye Yahathi alikuwa mkubwa wao, na Zina alikuwa wa pili; lakini Yeushi na Beria hawakuwa na wana wengi; basi wakawa mbari ya baba kwa kuhesabiwa pamoja.

12. Wana wa Kohathi; Amramu, Ishari, Hebroni, na Uzieli, watu wanne.

1 Nya. 23