39. na Azaria akamzaa Helesi; na Helesi akamzaa Eleasa
40. na Eleasa akamzaa Sismai; na Sismai akamzaa Shalumu;
41. na Shalumu akamzaa Yekamia; na Yekamia akamzaa Elishama.
42. Na wana wa Kalebu, nduguye Yerameeli, walikuwa Mesha, mzaliwa wake wa kwanza, aliyekuwa babaye Zifu; na wana wa Maresha, babaye Hebroni.
43. Na wana wa Hebroni; Kora, na Tapua, na Rekemu, na Shema.
44. Naye Shema akamzaa Rahamu, babaye Yorkeamu; na Rekemu akamzaa Shamai.
45. Na mwana wake Shamai alikuwa Maoni; na Maoni alikuwa babaye Bethsuri.
46. Naye Efa, suria yake Kalebu, alimzaa Harani, na Mosa, na Gazezi; naye Harani akamzaa Gazezi.
47. Na wana wa Yadai; Regemu, na Yothamu, na Geshani, na Peleti, na Efa, na Shaafu.
48. Naye Maaka, suria yake Kalebu, akamzalia Sheberi, na Tirhana.
49. Tena akamzaa Shaafu, babaye Madmana; na Sheva babaye Makbena; na babaye Gibea; naye binti Kalebu alikuwa Aksa.
50. Hao walikuwa wana wa Kalebu. Wana wa Huri, mzaliwa wa kwanza wa Efrathi; Shobali, babaye Kiriath-Yearimu;
51. Salma, babaye Bethlehemu; na Harefu, babaye Beth-gaderi.
52. Naye Shobali, babaye Kiriath-Yearimu, alikuwa na wana; Haroe, na nusu ya Wamenuhothi.