34. Basi huyo Sheshani alikuwa hana wana wa kiume, ila binti. Naye Sheshani alikuwa na mtumwa, Mmisri, jina lake akiitwa Yarha.
35. Basi akamwoza binti yake aolewe na Yarha, mtumwa wake; naye akamzalia Atai.
36. Na Atai akamzaa Nathani; na Nathani akamzaa Zabadi;
37. na Zabadi akamzaa Eflali; na Eflali akamzaa Obedi;
38. na Obedi akamzaa Yehu; na Yehu akamzaa Azaria;
39. na Azaria akamzaa Helesi; na Helesi akamzaa Eleasa
40. na Eleasa akamzaa Sismai; na Sismai akamzaa Shalumu;
41. na Shalumu akamzaa Yekamia; na Yekamia akamzaa Elishama.
42. Na wana wa Kalebu, nduguye Yerameeli, walikuwa Mesha, mzaliwa wake wa kwanza, aliyekuwa babaye Zifu; na wana wa Maresha, babaye Hebroni.
43. Na wana wa Hebroni; Kora, na Tapua, na Rekemu, na Shema.
44. Naye Shema akamzaa Rahamu, babaye Yorkeamu; na Rekemu akamzaa Shamai.
45. Na mwana wake Shamai alikuwa Maoni; na Maoni alikuwa babaye Bethsuri.