3. Wana wa Yuda; Eri, na Onani, na Shela; ambao hao watatu alizaliwa na binti Shua, Mkanaani. Naye Eri, mzaliwa wa kwanza wa Yuda, alikuwa mbaya machoni pa BWANA; naye akamwua.
4. Na Tamari, mkwewe, akamzalia Peresi, na Zera. Wana wote wa Yuda ni watano.
5. Wana wa Peresi; Hesroni, na Hamuli.
6. Na wana wa Zera; Zabdi, na Ethani, na Hemani, na Kalkoli, na Darda; hao wote ni watano.
7. Na wana wa Karmi; Akani, yule mwenye kutaabisha Israeli, aliyekosa katika kitu kilichowekwa wakfu.
8. Na wana wa Ethani; Azaria.
9. Tena wana wa Hesroni aliozaliwa; Yerameeli, na Ramu, na Kalebu.
10. Na Ramu akamzaa Aminadabu; na Aminadabu akamzaa Nashoni, mkuu wa wana wa Yuda;
11. na Nashoni akamzaa Salmoni; na Salmoni akamzaa Boazi;
12. na Boazi akamzaa Obedi; na Obedi akamzaa Yese;
13. na Yese akamzaa Eliabu, mzaliwa wake wa kwanza, na wa pili Abinadabu, na wa tatu Shama;
14. na wa nne Nethaneli, na wa tano Radai;
15. na wa sita Ozemu, na wa saba Daudi;
16. na maumbu yao ni Seruya, na Abigaili. Na wana wa Seruya walikuwa, Abishai, na Yoabu, na Asaheli; hao watatu.
17. Na Abigaili akamzaa Amasa; na babaye Amasa ni Yetheri, Mwishmaeli.