27. Na wana wa Ramu, mzaliwa wa kwanza wa Yerameeli, walikuwa Maasi, na Yamini, na Ekeri.
28. Na wana wa Onamu walikuwa Shamai, na Yada; na wana wa Shamai; Nadabu, na Abishuri.
29. Na mkewe Abishuri aliitwa jina lake Abihaili; naye akamzalia Abani, na Molidi.
30. Na wana wa Nadabu; Seledi, na Apaimu; walakini Seledi alikufa hana watoto.
31. Na wana wa Apaimu; Ishi. Na wana wa Ishi; Sheshani. Na wana wa Sheshani; Alai.
32. Na wana wa Yada, nduguye Shamai; Yetheri, na Yonathani; naye Yetheri akafa hana watoto.
33. Na wana wa Yonathani; Pelethi, na Zaza. Hao ndio wana wa Yerameeli.
34. Basi huyo Sheshani alikuwa hana wana wa kiume, ila binti. Naye Sheshani alikuwa na mtumwa, Mmisri, jina lake akiitwa Yarha.
35. Basi akamwoza binti yake aolewe na Yarha, mtumwa wake; naye akamzalia Atai.
36. Na Atai akamzaa Nathani; na Nathani akamzaa Zabadi;
37. na Zabadi akamzaa Eflali; na Eflali akamzaa Obedi;
38. na Obedi akamzaa Yehu; na Yehu akamzaa Azaria;